Skip to main content

SHIVYAWATA YAOMBWA KUFANYA VIKAO NA WATU WENYE ULEMAVU MARA KWA MARA

                                  Image result for SHIVYAWATA





Shirikisho la watu wenye ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) limeombwa kuitisha na kufanya vikao vya mara kwa mara ili kujadili mambo mbalimbali yanayohusiana na walemavu.

Rai hiyo imetolewa na Mjumbe wa kamati ya watu wenye ulemavu mkoa wa Dodoma ambaye pia ni fundi mkuu katika karakana ya kutengeneza vifaa visaidizi kwa watu wenye ulemavu wa viungo jijini Dodoma (KAWADO) Bwana MWITA MARWA wakati akizungumza na Dodoma FM.

Bwana Marwa amesema shirikisho hilo litakapoweka utaratibu wa kukutana mara kwa mara itasaidia watu wenye ulemavu kuweka mipango itakayowasaidia  ikiwa ni pamoja na kujadili namna ya kupata ufadhili jambo ambalo litawasaidia kujikwamua kiuchumi.

Amesema kutofanya vikao kwa washirika katika shirikisho hilo kunapelekea kila mmoja kuanzisha mradi wake binafsi jambo ambalo linapelekea baadhi yao kukwama kutokana na uwezo wa mitaji huku akisema changamoto hizo zinaweza kupungua kama watakuwa na utaratibu wa kukaa kwa pamoja na  kujadili.

Fundi huyo mkuu wa (KOWADO) amesema kwa kuzitambua changamoto za walemavu  wa viungo jijini Dodoma karakana hiyo ilianza kutengeneza vifaa visaidizi mbalimbali kwa ajili ya walemavu wa viungo kama baiskeli na kuingia tenda za kutengeneza vifaa hivyo kwa watu nje na walemavu na hata serikalini japo amesema changamoto kubwa ikiwa ni uwezeshwaji.

Hata hivyo ameiomba serikali kuwapa kipaumbele walemavu kwa kuwawezesha katika shughuli wanazozifanya kingine ikiwa ni kuwatengenezea mazingira ya kufika sehemu husika kwa urahisi mfano baadhi ya ofisi zilizokojuu zimekuwa hazina lifti jambo ambalo ni changamoto kwao.

Na RWEIKIZA KATEBALIRWE                                    DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...