Skip to main content

SHIRIKA LA PELUM TANZANIA LAPUNGUZA MIGOGORO YA ARDHI WILAYA YA KONGWA DODOMA

Image result for shirika la PELUM TANZANIA



Wananchi wilayani kongwa wametakiwa kutumia mafunzo wanayopatiwa na mashirika mbalimbali yasiyo ya kiserikali kuleta maendeleo kwa kutambua matumizi sahihi ya mpango wa matumizi ya aridhi pamoja na kuhakikisha wanatatua migogoro sugu ya ardhi katika maeneo yao.
Wito huo umetolewa leo na Diwani wa kata ya kongwa Bwana White Zubery wakati akifungua mdahalo wa haki za ardhi wilayani kongwa wenye lengo la kutambua usimamizi wa mpango wa matumizi sahihi ya ardhi na uundwaji wa vyombo vya utatuzi wa migogoro ya ardhi vijijini unaotekelezwa na shirika la PELUM TANZANIA katika wilaya za Kongwa na Bahi Jijini Dodoma.
Amesema kuwa ni vyema wananchi wakatumia mafunzo hayo kwani awali katika vijiji kama vya Lenjulu , chilangilizi ,Iduo na Suguta kulikuwa na migogoro mingi inayohusisha wakulima na wafugaji ambapo kupitia mafunzo yanayotolewa na shirika la PELUM TANZANIA maeneo mengi migogoro hiyo imetatuliwa.
Aidha amewataka kutumia mafunzo hayo kwa manufaa ya wananchi wengine walioko katika maeneo mbalimbali ya nje na wilaya hiyo na kuacha kuitegemea serikali ifanye kila jambo.
Awali akitoa taarifa fupi mbele ya mgeni rasimi afisa mradi kutoka shirika la PELUM TANZANIA Bi Anna Marwa  Amesema kuwa wameamua kutoa mafunzo hayo kwa lengo la kuwajengea viongozi na wananchi uelewa mkubwa ili kutambua sheria mbalimbali zinazohusu masuala ya ardhi ambapo amedai baada ya mafunzo hayo kutolewa migogoro ya ardhi imepungua kwa asilimia 70 katika wilaya ya Kongwa.
Nao baadhi ya wananchi walioshiriki katika mdahalo huo wamelipongeza shirika hilo kwa kutoa mafunzo hayo  kwani mradi huo umewasaidia kutambua sheria mbalimbali ambazo zimekuwa zikiwasaidia katika kutatua migogoro ya ardhi pamoja na ile ya wakulima na wafugaji.
Shirika la PELUM TANZANIA lenye makao makuu yake mkoani Morogoro linatekeleza mradi wa ushiriki wa wananchi katika kusimamia sekta ya kilimo na unatekelezwa katika mikoa mitatu na wilaya sita ambayo ni Morogoro ,Iringa na Dodoma ambapo katika mkoa wa Dodoma unatekelezwa katika wilaya ya bahi na Kongwa ndani ya vijiji 30.
Na Alferd Bulahya                                          Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...