Serikali imekutana na wadau wa Maendeleo Jijini
Dar es Salaam kujadiliana kuhusu utekelezaji wa Sera na Mipango ya kitaifa
inayohusu masuala ya jinsia ikiwemo Mpango wa Kitaifa wa Kutokomeza
vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (2017/18
– 2021/22).
utekelezaji wa mikataba ya kikanda na kimataifa
kuhusu kufikia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi.
Akizungumza katika kikao kati ya Serikali na wadau hao Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Nkinga amesema Serikali imeamua kukutana na wadau ili kujadiliana na kupata maoni kuhusu utekelezaji wa Sera Mipango na mikakati ya Serikali katika masuala ya kijinsia ili kuweza kutekeleza kwa mafanikio masuala hayo.
Ameongeza kuwa Serikali inashirikiana na wadau wa Maendeleo kwa karibu ili kuwa na Mipango na mikakati ya pamoja ya kutekeleza masuala mbalimbali ya kijinsia ikiwemo kutokomeza vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto na uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi.
"Ni jambo la busara kuwashirikisha wadau wa Maendeleo katika masuala ya kimaendeleo ili kupeleke mbele kurudumu la maendeleo" alisisitiza Bi. Sihaba.
Akizungumza katika kikao kati ya Serikali na wadau hao Katibu Mkuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Sihaba Nkinga amesema Serikali imeamua kukutana na wadau ili kujadiliana na kupata maoni kuhusu utekelezaji wa Sera Mipango na mikakati ya Serikali katika masuala ya kijinsia ili kuweza kutekeleza kwa mafanikio masuala hayo.
Ameongeza kuwa Serikali inashirikiana na wadau wa Maendeleo kwa karibu ili kuwa na Mipango na mikakati ya pamoja ya kutekeleza masuala mbalimbali ya kijinsia ikiwemo kutokomeza vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto na uwezeshaji wa Wanawake kiuchumi.
"Ni jambo la busara kuwashirikisha wadau wa Maendeleo katika masuala ya kimaendeleo ili kupeleke mbele kurudumu la maendeleo" alisisitiza Bi. Sihaba.
Akizungumzia utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Kutokomeza
vitendo vya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (2017/18 – 2021/22)(NPA) Kaimu Mkurugenzi
Idara ya Sera na Mipango kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto Bw. Atupele Mwambene amesema kuwa Serikali imetekeleza Mipango
huo kwa mafanikio tangu kuzinduliwa kwake na masuala mbalimbali
yametekelezwa katika Mipango huo ikiwemo kuwawezesha maafisa Maendeleo ya Jamii
na Ustawi wa Jamii kutoa elimu juu ya vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na
Watoto iliyosaidia kupunguza vitendo hivyo hasa katika maeneo ya vijijini.
Kwa upande wake Muwakilishi wa UN Women nchini Bi. Susan Steffen akizungumza kwa niaba ya wadau wa Maendeleo ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuwashirikisha katika masuala mbalimbali ya Maendeleo na kuahidi kuendelea kushirikiana katika masuala mbalimbali kwa manufaa ya taifa la Tanzania.
Na Mariam
Matundu DODOMA
FM
Comments
Post a Comment