Skip to main content

SERIKALI YAKIRI KUWALIPA MAWAKALA WA KILIMO AMBAO WALIWAKOPESHA 2014/2015

                       Image result for naibu waziri wa kilimo Dr Mery





Serikali imesema katika kipindi cha mwaka wa fedha 2014/15 iltoa ruzuku ya pembejeo za kilimo kupitia vikundi vya wakulima pamoja na Bank jamii badala ya utaratibu wa vocha za pembejeo zilizokuwa zikitumika hapo awali.

Naibu Waziri wa kilimo Dr. Merry Mwanjelwa ameyabainisha hayo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge Jackline Ngonyani aliehoji ni lini Serikali itawalipa mawakala wa kilimo ambao waliikopesha Serikali tangu mwaka 2014/15.

Amesema utaratibu huo ulitumika ili kuwajengea uwezo wa kulima kuto kukopa na kujipatia pembejeo wao wenyewe na Serikali ilitakiwa kuchangia 20% ya gharana za pembejeo kwa hekali moja utaratibu uliopangwa kutumika Nchi nzima lakini Mikoa Morogoro, Njombe, Iringa Manyara, Mbeya Ruvuma Rukwa na Tabora ndio iliyotekeleza agizo hilo

Naibu waziri huyo amesema uhakiki wa awali ulifanyika katika Mikoa ipatayo kumi, na kupitia uhakiki huo imejiridhisha kuwepo kwa mapungufu katika baadhi ya makampuni na mawakala ikiwemo kukosekana kwa nyaraka za manunuzi, kuto kuwepo kwa mikataba ya kazi, kukosekana kwa orodha ya wakulima wanufaika katika vijiji husika.

Ameongeza kuwa Serikali itaboresha sekta ya kilimo Nchini kupitia malipo kwa mawakala na uhakiki ukiwa bado unaendelea baada ya kukamilika taarifa rasmi itatolewa ili kukamilisha malipo hayo..

Na Pius Jayunga                                      Bunge/Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...