Skip to main content

SERIKALI YAENDELEZA MIPANGO YA KITAIFA YA MAFUNZO KWA VITENDO KWA WAHITIMU

Image result for Mbunge wa Dodoma Mjini





Serikali kupitia ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi Ajira na watu wenye ulemavu imeandaa muogozo wa kitaifa wa mafunzo ya vitendo kwa wahitimu wa elimu ya juu pamoja na vyuo vya ufundi ili kusaidia wadau kuandaa, kusimamia, pamoja  na kuratibu mafunzo ya uzoefu kazini kwa wahitimu.

Hayo yamebainishwa leo Bungeni Jijijini Dodoma na  Naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu Mh. Anthony Mavunde wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Zainabu Athumani Katimba  aliehoji Serikali haioni haja ya kutungwa kwa sera ya mafunzo kwa vitendo kazini kwa wahitimu wa elimu ya juu na vyuo vya ufundi ili vijana waweze kupata ujuzi utakaoendana na soko la ajira.

Akijibu swali hilo Mavunde amesema Serikali imeona kuna haja ya kuandaa miongozo ya kitaifa ya kisera ya mafunzo kwa vitendo kwa wahitimu wa ngazi mbalimbali mwongozo uliozinduliwa mwezi septemba mwaka 2017 na kuanza kutumika rasmi katika mwaka wa fedha 2017/18 ambapo zaidi ya nafasi 750 zimetolewa na waajiri pamoja na kufanya mafunzo kwa vitendo.

Aidha Mavunde amesema baada ya kupitishwa kwa sera hiyo swala la mafunzo kwa vitendo kwa wahitimu litawekwa katika sheria ya ajira na mahusiano kazini ya mwaka 2004 na kupitia mkutano huo Mh. Mavunde ametoa wito kwa wa ajiri Nchini kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa mpango wa mafunzo kazini katika maeneo yao ya kazi.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri mkuu sera, bunge, kazi, ajira na wenye ulemavu Mh. Jenister Mhagama amesema kazi kubwa ya ofisi ya Waziri mkuu ni kuungana na wadau wa Wizara ya elumu kupitia vyuo vikuu Nchini ili kuwaandaa vijana wahitimu wa elimu ya juu kuingia katika soko la ajira.

Katika mkutano huo jumla ya maswali kumi yameulizwa na Waheshimiwa. Wabunge na kisha kutolewa majibu kupitia wizara husika.

Na Pius Jayunga                                                        DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...