Skip to main content

SERIKALI NA WADAU WAJIPANGA KUDHIBITI UKATILI WA WATOTO MITANDAONI

Image result for Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Marcel Katemba




Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imedhamiria kumlinda mtoto dhidi ya ukatili ukiwemo unyanyasaji wa mtandaoni.

Katika kulifanikisha hilo Wizara imekutana na wadau wa maendeleo ya mtoto Jijini Dodoma kujadili kuhusu namna bora ya kupambana na ukatili wa mtoto mtandaoni ambao unaenea kwa kasi kubwa na kutishia hatima ya watoto na jamii kwa ujumla.

Akifungua kikao kati ya Serikali na wadau wa Maendeleo ya Mtoto Kaimu Katibu Mkuu Idara Kuu Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Marcel Katemba amesema kuwa Serikali haitafumbia macho matumizi ya mitandao ambayo yana athari mbaya kwa watoto ili kuhakikisha kuwa kunakuwepo udhibiti wa matumizi ya mitandao ili kuwalinda watoto dhidi ya unyanyasaji wa kingono mtandaoni.

Bw. Marcel Katemba ameleza kuwa Serikali inatambua mchango wa wadau katika mapambano dhidi ya ukatili wa kingono kwa watoto mitandaoni, hivyo kwa pamoja watashirikiana kuhakikisha kuwa vita ya kupambana na ukatili dhidi ya Mtoto ikiwemo ukatili wa mtandaoni inafanikiwa.

Ameongeza kuwa Serikali inatambua mchango wa wadau katika ulinzi na usalama wa watoto na Serikali itaendelea kushirikiana na wadau ili kupata mbinu na namna sahihi za kupambana na ukatili ili kulinda watoto wetu dhidi ya madhara ya matumizi maovu ya mitandao.

Kwa upande wake  Mhadhiri wa Chuo cha Ualimu Dar es salaam (DUCE) Dkt. Hezron Onditi akiwasilisha utafiti kuhusu hali ya ukatili wa mtoto mtandaoni, amesema kuwa tatizo la ukatili wa mtandaoni kwa watoto ni kubwa na linaenea kwa kasi na mpaka sasa takribani asilimia ya 5 – 72 ya watoto na vijana wadogo duniani wamefanyiwa ukatili wa kingono mtandaoni ikilinganishwa na asilimia 58 ya watoto waliofanyiwa ukatili huo kupitia matumizi ya simu na mitandao hapa nchini.

Naye Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mtoto Bi. Magreth Mussai amesisitiza kuwa wazazi na walezi na jamii kwa ujumla wanatakiwa kuzingatia na kuimarisha malezi ya watoto katika mazingira ya shule na majumbani ili kuzuia athari mbaya zinazosababishwa na matumizi mabovu ya simu na mitandao katika dunia ya teknolojia na utandawazi.  

MARIAM MATUNDU                                                 DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...