Skip to main content

SERIKALI KUTOA ELIMU YA UGONJWA WA HOMA YA INI

                     
Image result for NAIBU WAZIRI WA AFYA





Serikali kupitia wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto imejipanga kuongeza juhudi za kufikisha elimu kwa wananchi ili kuzitambua njia za kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa homa ya ini licha ya kuwepo kwa juhudi zinazoendelea kufanyika.

Naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dr. Faustine Ndugulile ametoa ufafanuzi huo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge Mh. Felister Aloyce Bura alietaka kujua Serikali inamkakati upi wa kutoa elimu kwa wananchi ili kujiepusha na maambukizi ya ugonjwa huo.

Amesema wizara ya afya kupitia vitengo vyake vya elimu kwa umma  imekuwa ikiandaa majalinda pamoja na machapisho mbalimbali kwa ajili ya kuifikishia jamii elimu ya kujikinga na ugonjwa huo pamoja na kutembelea katika cliniki mbalimbali ili kuwafikia wananchi kwa urahisi zaidi.

Amesema virusi vya ugonjwa wa ini vimegawanyika katika makundi matano na tofauti yake ni katika uambukizaji ambapo virusi vya kundi BC na D maambukizi yake ni sawa na yale ya virusi vya ukimwi kupitia njia ya kujamiiana, kuongezewa damu huku virusi vya kundi A na kundi E ikiambukiza kwa njia ya unywaji wa maji yasiyokuwa safi na salama.

Akielezea dalili za ugonjwa wa homa ya Ini Dr. Ndugulile amesema mgonjwa huanza kuonekana akiwa na  rangi ya njano katika ngozi na macho, kujisaidia haja ndogo iliyo na rangi nyeusi, joto la mwili kupanda, kupata mafua, kichwa kuuma, kupata kichefuchefu, kutapika pamoja na tumbo kuuma upande wa juu kulia.

Na Pius Jayunga                                            Bunge/DODOMA  FM


Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...