Skip to main content

SERIKALI KUJENGA MAJENGO BORA KATIKA MAJIJI YOTE NCHINI IKIWEMO DODOMA

             
                                 Image result for WAZIRI MKUU KASIMU






Serikali imesema itahakikisha inajenga majengo mazuri katika majiji yote nchini ikiwemo jiji la Dodoma ili kukabiliana na changamoto ya ujenzi holela .

Hayo yamebainishwa leo na waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania MH Kassimu Majaliwa wakati akifungua warsha ya siku mbili kwa wabunifu majengo na wakadiriaji  yenye lengo la kutoa mafunzo ya kuendeleza ujenzi wa majengo ya kitaalamu pamoja na miundo mbinu mipya.

Amesema kuwa wakati serikali ikiendelea kujenga miundo mbinu mipya hasa  katika jiji la dodoma bado pia itaendelea kuyaboresha majengo yaliyopo katika majiji yote ambayo ni Mbeya, Mwanza Tanga na Arusha na itahakikisha haifanyi makosa kama yaliyofanyika katika ujenzi wa jiji la Dar es salaam.

Aidha ameongeza kuwa kwa mwaka huu bodi ya wabunifu wa majengo na wakadiliaji wa majenzi itaandaa michoro kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya kata katika ngazi za kata na amewataka wataalu kusimamia kikamilifu ujenzi huo ili kupata majengo na vituo bora vya afya nchini kote.

Kwa upande wake waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Makame mbarawa amesema kuwa ili kukabiliana na changamoto ya upungufu wa rasilimali fedha wizara imetenga kiasi cha shilingo milioni 50 kwa ajili ya zoezi hilo kwa mwaka huu na katika bajeti ijayo ya mwaka wa fedha 2018/19 jumla ya shilingi milioni 100 zimetegwa ili kuondoa mapungufu yaliyopo.

Alfred Bulahya                                                     DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...