Skip to main content

SERIKALI IMETOA ZAIDI YA BILIONI 30 KWA AJILI YA MADAI YA WALIMU

                      Image result for josephat kandege





Katika kipindi cha mwezi June 2015 hadi Desemba 2017 Serikali imetumia kiasi cha shilingi bilioni 33.135 kulipa  madai ya walimu wapatao 86,234 Nchi nzima.

Naibu Waziri ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za mitaa TAMISEM Mh. Josephat Kandege ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge Hussen Nassoro Amary aliyehoji ni lini walimu wataboreshewa masilahi yao na nyumba za kuishi.

Amesema Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuboresha masilahi ya walimu Nchini ikiwemo ujenzi wa nyumba za walimu pamoja na miundombinu mingine ya shule na kwamba ili kufanikisha swala hilo viongozi mbalimbali wakiwemo wabunge ni wadau wakubwa katika kuunga mkono juhudi hizo.

Naibu Waziri huyo amesema kupitia sheria namba 25 ya mwaka 2015 ilianzisha tume ya utumishi ya walimu ili iweze kusimamia na kushughulikia masuala yahusuyo masilahi ya walimu na katika kuhakikisha masilahi ya walimu yanaboreshwa na kero zao kuondolewa jumla ya walimu 52 katika Halimashauri ya Wilaya ya Nyang’wale walilipwa jumla ya sh. Milioni 99,685,990 za madai mbalimbali.

Mh. Kandege amesema katika Mkoa wa Kagera una mahitaji ya vyumba vya madarasa 14,275 kwa shule za msingi, mahitaji ya ofisi za walimu 1780, na katika shule za sekondari vyumba vya madarasa vikihitajika 2,379, majengo ya utawala yakihitajika 212 changamoto ambazo Serikali inaendelea kuzifanyia kazi kutokana na ongezeko la watoto kuandikishwa shuleni.

Na Pius Jayunga                                                   Bunge/Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...