Serikali imeanza
mchakato wa kuandaa kitini cha masuala ya jinsia kuendeleza kasi ya utekelezaji
wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Akizungumza katika
kikao cha wataalam na wadau wa maendeleo ya Jinsia Mwakilishi wa Mkurugenzi wa
Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bi. Mboni Mgaza amesema Ukatili dhidi ya Wanawake
na Watoto umekithiri sana nchini hivyo
Serikali kuamua kutafuta njia tofauti za kupambana na tatizo hilo.
Amesema lengo la kuandaa kitini cha kufundishia
masuala ya Jinsia “ni kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa
kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ambao utatoa uelewa kwa wadau wa
maswala ya jinsia na maafisa Maendeleo ya Jamii kuanzia ngazi ya Mkoa,
Halmashauri na kata ili kutoa elimu ya masuala ya Jinsia katika jamii.
Bi. Mboni amefafanua
kuwa kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya
wanawake nchini ilikuwa ni Milioni Ishirini na Tatu na Elfu Hamsini na nane Mia
tisa Thelathini na tatu sawa na asilimia 51.3 ya watanzania na ndio wanaokumbwa
na vitendo vya ukatili kwa kiasi kikubwa.
Amesisitiza kuwa kitni
hicho kitazingatia masuala mbalimbali kama vile lugha na mazingira ya walengwa
hasa wa vijijini ili kiweze kuleta matokeo mazuri katika kupambana na ukatili
dhidi ya wanawake na watoto nchini.
Mariam Matundu Dodoma FM
Comments
Post a Comment