Watu wenye magonjwa
sugu ikiwemo ugonjwa wa saratani ya kizazi wametajwa kuwa hatarini kushuka
kwa kinga ya mwili hivyo kupelekea
kuruhusu vimelea wengine kushambulia mwili wa binadamu.
Hayo yamebainishwa
na Daktari wa magonjwa ya wanawake
kutoka hospitali ya Makole mjini Dodoma Dokta
Antony Sangana wakati akizungumza na Dodoma FM ambapo amesema kushuka kwa kinga
ya mwili husababishwa na vitu vingi ikiwa ni pamoja na ugonjwa wa saratani.
Amesema wakati saratani
ya kizazi ikiwa inashambulia kwenye mwili kwa kiwango kikubwa inapelekea
kushuka kwa kinga ya mwili hivyo kupelekea vimelea kushambulia mwili.
Ametaja ugonjwa wa
kisukari endapo utashindwa kudhibitiwa
ni miongoni mwa ugonjwa unaoweza kusababisha kupungua kwa kinga ya mwili
huku akiwataka waathirika wenye ugonjwa huo kwenda katika vituo vya afya mapema
na kupatiwa matibabu.
Hata hivyo wananchi
wameshauriwa kutumia vyakula vye vitamin B ambavyo vimetajwa kuwa na uwezo wa
kupambana na vimelea vinavyo sababisha magonjwa mwilini na kulinda kinga ya
mwili.
Serikali ya Tanzania imezindua kampeni ya chanjo ya
kuzuia saratani ya shingo ya kizazi huku ikikadiriwa kuwa zaidi ya wasichana laki 6 walio na umri kati
ya miaka 9 hadi 14 watachanjwa nchini nzima.
Na Benard
Filbert
Dodoma FM
Comments
Post a Comment