Skip to main content

SABABU ZINAZOPELEKEA WAKULIMA KUUZA MAZAO YAO KWA WALANGUZI NI HIZI

Elimu ndogo dhidi ya watendaji pamoja na kutokuwepo uaminifu na migogoro ndani ya vyama vya msingi vya ushirika imetajwa kuwa chanzo cha kupelekea wakulima kuuza mazao yao kwa walanguzi badala ya kuuza katika vyama hivyo.


Kauli hiyo inakuja baada ya serikali kutakiwa kuweka mipango mikakati mizuri ya kuhakikisha mkulima anauza mazao yake katika vyama vya msingi na kuepukana kuwauzia walanguzi jambo ambalo linachangia kutonufaika na mazao yake.

Akizungumza na Dodoma FM juu ya suala hilo mkurugenzi wa shirika la usimamizi na ukaguzi wa vyama vya msingi COASCO Tanzania bwana SAAD WADAA amesema kuwepo na watendaji wenye elimu ndogo katika vyama hivyo husababisha  utendaji mbaya katika kuhudumia wahitaji huduma na hivyo chama kubezwa na wananchi  kingine ikiwa ni baadhi ya watendaji kuingia katika nyazfa za uongozi kwa maslahi binafsi.

Bwana WADAA amesema jambo jingine linalofanya wakulima wasiuze mazao yao katika vyama hivyo ni kuwepo kwa migogoro baina ya viongozi jambo ambalo amesema hapo nyuma lilikuwa likichangiwa na maswala ya kisiasa.

Aidha mkurugenzi huyo amesema wao wakiwa wakaguzi na wasimamizi wamekuwa wakitatua migogoro ambayo iko chini yao kwa mjibu wa sheria huku migogoro inayohusiana na ubadhirifu wa fedha ikitatuliwa na  vyombo vingine kama polisi na Takukuru.

Hata hivyo amewataka wananchi kuwa makini wanapofanya uchaguzi wa viongozi wa vyama vya msingi kwa kuzingatia sifa alizonazo mhusika ili kuleta ufanisi wa kazi katika vyama hivyo jambo ambalo litaepusha migogoro isiyo ya lazima.

Na RWEIKIZA KATEBALIRWE                                  DODOMA  FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...