Skip to main content

RC MAHENGE ASEMA UTARATIBU WA KUUNGANISHA MIFUKO YA JAMII UKO VIZURI

                     Image result for MKUU WA MKOA WA DODOMA BINILITHI                   


MKUU wa mkoa wa Dodoma,Dk.Binilithi Mahenge amewahakikiasha wafanyakazi wote kuwa utaratibu wa kuunganisha mafao yao upo vizuri na hakuna mafao ya wafanyakazi yatakayopotea kutokana na mafao hayo kupelekwa katika mfuko husika.

Akizungumza katika maadhimisho ya sherehe za Wafanyakazi (Mei Mosi zilizopambwa na maandamano mbalimbali ambayo yamefanyika jijini Dodoma katika uwanja wa jamuhuri huku kauli mbiu ikiwa ni kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii nchini ukilenga kuboresha mafao ya wafanyakazi.

DK BINILITH MAHENGE Amesema ujumbe huo una lengo la kuijulisha serikali kama msimazi mkuu wa sheria ya ajira ikiwemo haki za wafanyakazi na moja ya sera ya serikali imelenga kutoa haki kwa wananchi wote pamoja na watumishi.

Akisoma risala kwa niaba ya wafanyakazi mjumbe wa kamati ya utendaji TUICO mkoa GODFREY NDOSHI, amesema kuwa
wafanyakazi wanakabiliana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwa na mishahara midogo ambayo wakati mwingine wafanyakazi wanashindwa kufikia malengo.

Katika hatua nyingine NDOSHI,  ameongeza  kuwa serikali inatakiwa
kuwawajibisha waajiri ambao wamekuwa na tabia ya kuchelewesha makato ya watumishi au kutolipa kabisa katika mifuko ya jamii jambo ambalo linasababisha kuwepo kwa malalamiko kati ya mfuko, mwajiri na mwajiriwa.

Nchini Tanzania Maadhimisho ya Mei Mosi  kitaifa yameadhimishwa katika mkoa wa iringa.
Na,Mindi Joseph                                                                   Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...