Skip to main content

RAIS MAGUFULI AELEZEA LENGO LA SERIKALI KUWEKEZA KATIKA UJENZI WA MIRADI MBALIMBALI

                                   Image result for rais magufuli azindua barabara ya kondoa



Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amesema lengo la serikali kuwekeza katika ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo Nchini ni kujenga mazingira mazuri ya kuboresha masilahi ya watumishi wa umma katika siku za usoni.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi MEI MOSI  yaliyofanyika kitaIfa katika Mkoa wa Iringa na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali akiwemo Waziri mkuu Kasimu Majaliwa.

Amesema fedha ambazo zimekuwa zikitolewa na Serikali kufanikisha mpango wa elimu bila malipo kwa wanafunzi kiasi cha shilingi bil. 23.8, mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kiasi cha shilingi bil. 483 inalenga kunufaisha pande zote kuliko kutumia fedha hizo kujiongezea mishahara inayonufaisha upande mmoja wa watanzania.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli amesisitiza suala la malipo kwa mfanyakazi pale anapohamishwa kituo cha kazi kupatiwa stahiki zake na kwamba zoezi hilo linapaswa kusimamiwa kikamilifu na waajiri katika maeneo yote Nchini.

Kwa upande wake katibu mkuu wa TUCTA Nchini Dr. Yahaya Msigwa amesema chama cha wafanyakazi Nchini TUCTA hakita kubali kuwavumilia wafanyakazi wazembe, wavivu na wale wasio kuwa na nidhamu na kwamba vitendo vya rushwa vitaendelea kukemewa miongoni mwa wafanyakazi.

Na Pius Jayunga                                                                Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...