Skip to main content

RAIS MAGUFULI AELEZA NAMNA SERIKALI ILIVYOONGEZA BAJETI WIZARA YA AFYA


Image result for RAIS MAGUFULI



Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Mgufuli amesema Serikali imejitahidi kuongeza bajeti ya Wizara ya afya kwa sehemu kubwa kila mwaka kwa lengo la kuboresha huduma za afya na kuwafikia wananchi kwa urahisi.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo wakati akiweka jiwe la msingi la Ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Kilolo iliyopo Mkoani Iringa na kueleza kuwa jitihada hizo ni utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi kuboresha huduma za afya Nchini.

Amesema kwa mwaka 2015/16 bajeti ilikuwa Trilioni 1.8 na mwaka 2016/17 bajeti ikaongezeka hadi kufikia Trilioni 2.2 zote zikipelekwa katika sekta ya afya ambapo kwa sasa vituo vya afya zaidi ya 208 vimejengwa na vingine vikikarabatiwa huku mkakati uliopo ikiwa ni kujenga hospitali za wilaya 67.

Aidha Rais Magufuli ametumia fursa hiyo kutoa wito kwa wananchi kujiunga katika mifuko ya bima ya afya ili kunufaika na huduma za matibabu pale mwanachama anapougua ikiwa ni pamoja na Wizara ya afya kuendelea kuhamasisha wananchi kujiunga kwa wingi ili kurahisisha upatikanaji wa huduma za afya.

Kwa upande wake Waziri wa Tamisem Mh. Seleman Jafo amesema tayari kamati ya Bunge imekwisha fanya ziara ya kukagua ujenzi wa Hospitali hiyo na kurizishwa na hatua za ujenzi wake na baada ya kukamilika ujenzi wa Hospitali hiyo itakuwa msaada mkubwa kwa wakazi wa Wilaya ya Kilolo.

Na Pius Jayunga                                                    Dodoma FM Radio

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...