Skip to main content

RAIS MAGUFULI AAGIZA BILIONI 2 ZILIZOELEKEZWA UDSM ZIPELEKWE SOKOINE ZIJENGE MABWENI

            Image result for RAIS MAGUFULI




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli ameagiza fedha kiasi cha sh. bil. 2 zilizoelekezwa katika chuo kikuu cha Dar es salaam zitumike kujenga mabweni ya chuo kikuu cha Sokoine kilichopo Mkoani Morogoro.

Rais Magufuli ametoa maagizo hayo leo akiwa Mkoani Morogoro wakati akizungumza na wananchi pamoja na wanafunzi wa chuo kikuu cha Sokoine baada ya kupokea malalamiko ya wanafunzi hao likiwemo suala la upungufu wa mabweni hatua inayolazimu wengi wao kuishi mbali na eneo la chuo.

Rais Magufuli amesema pamoja na changamoto zilizowasilishwa na wanafunzi hao bado Serikali inatambua mchango wa chuo hicho katika kuboresha sekta ya kilimo Nchini na kuagiza fedha hizo kiasi cha shilingi bilioni. 2 zitumike kwa ujenzi wa mabweni ili kuondoa.

Katika hatua nyingine Rais Magufuli ameonesha kufurahishwa na hatua zilizofikiwa na chuo cha Sokoine ikiwemo kufanya utafiti wa panya kugundua mahali ambapo limefichwa bomu na kuahidi kuongeza idadi ya trekta zipatazo kumi chuoni hapo kwa lengo la

Kwa upande wake Waziri wa elimu sayansi na teknolojia Prof. Joyce Ndalichako amesema chuo hicho kimefanikiwa kuvumbua mbegu za matunda aina ya papai zaidi ya 4000 zenye uwezo wa kukomaa na kutoa matunda ndani ya miezi mitano, mbegu zingine ikiwa ni mpunga pamoja na maharage.

Na Pius Jayunga                                                     Dodoma FM


Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...