Skip to main content

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU IMETOA MAFUNZO KWA WAANDAAJI NA WATUMIAJI WA TAKWIMU ILI KUBORESHA UTOAJI TAKWIMU SAHIHI



Image result for TAKWIMU ZA JINSIA






Shirika la umoja wa mataifa linalojihusisha na usawa wa kijinsia  na maendeleo kwa wanawake lipo katika  mpango wa kuendeleza TAKWIMU  za kijinsia likiwa na lengo la kufahamu idadi ya wanawake pamoja na wasichana waliopo kote nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dodoma Katika Ofisi za CAG kupitia Warsha iliyoandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu muwakilishi kutoka shirika hilo Bi. USU MARYA amesema mpango huo unaenda sambamba na malengo yaliyopo kwenye mkakati wa nchi wa miaka mitano ambao una lengo la kuiendeleza nchi kwa kufahamu Takwimu katika sekta  mbalimbali nchini.

Aidha Bi. USU amesema kuwa kuna haja kubwa ya kuweka mikakati ya  kufanya uchambuzi wa ziada ambao utasaidia kupata idadi kamili ya wanawake wa vijijini na mijini pamoja na wanaume ili kusaidia Taasisi pamoja na Wizara husika kujua Takwimu za kijinsia.

Nae Meneja wa Takwimu za Mazingira na Uchambuzi ambae pia ni mshirika wa uratibu wa utekelezaji wa Takwimu kwa ajili ya kupima utekelezaji wa mpango wa pili wa maendeleo ya taifa BI. RUTH MINJA amesema ofisi ya Taifa ya Takwimu inashirikiana  na wadau ili kutoa Takwimu zitakazosaidia mipango mingine ya maendeleo kwa jamii.

Ukusanyaji wa Takwimu katika sekta mbalimbali ni moja ya sababu inayopelekea kuwepo kwa maendeleo katika sekta husika pamoja kukua kwa uchumi wa nchi kwa kufahamu idadi na malighafi zilizopo nchini.

Na ANIPHA RAMADHANI                                       DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...