Skip to main content

NAIBU WAZIRI WA AFYA ATOA MAAGIZO MAZITO HOSPITALI YA RUFAA DODOMA



Image result for waziri ndugulile




Serikali kupitia Wizara ya Afya imewataka viongozi wote wanaosimamia utoaji huduma katika hospital ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma kuhakikisha huduma ya x ray inapatikana ndani ya mwezi mmoja ili kuwasadia wagonjwa wenye uhitaji wa huduma hiyo .

Naibu waziri wa Wizara ya afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto dokta Faustine Ndugulile ametoa kauli hiyo leo alipofanya ziara ya ukaguzi  hospitalini hapo ambapo ameshuhudia wagonjwa wakikosa huduma ya x ray kwa muda wa wiki tatu sasa.

Amesema kuwa licha ya kuwepo kwa mashine mpya kwa ajili ya huduma hiyo bado wananchi wamelazimika kukosa huduma hiyo katika mkoa wote wa Dodoma kutokana na mashine iliyokuwa ikitoa huduma kuharibika hivyo ni wajibu wa viongozi wote wanaohusika kuhakikisha wanashughulikia tatizo hilo ili huduma ziendelee.

Aidha amewataka watumishi wote kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wagojwa na kuacha tabia ya kutoa lugha za matusi kwani zipo taarifa zinazodai kuwepo kwa baadhi ya watumishi wanaotoa lugha chafu kwa wagonjwa jambo ambalo halikubaliki.

Kwa upande wake mwenyekiti ya bodi ya usimamizi wa hospitali hiyo Dokta Job Lusinde amesema kuwa licha ya changamoto hiyo bado ipo changamoto nyingine ya kukosa duka la dawa la hospitali pamoja na nyumba ya kupumzika kwa upande wa akina mama licha ya kuhudumia wagonjwa wengi wakiwemo wanaotoka katika mikoa mingine jirani.

NA ALFRED BULAHYA                                                       DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...