Skip to main content

MWILI WA ALIYEKUWA MBUNGE WA BUYUNGU WAAGWA LEO BUNGENI JIJINI DODOMA

                                             
Image result for KUUAGA MWILI WA MBUNGE WA KAKONKO






Wizara ya mambo ya ndani ya nchi kupitia idara ya wahamiaji imefanikiwa kukamata Jumla ya wahamiaji haramu 13,393 katika kipindi cha Mwezi July 2017 hadi March 2018.

Naibu Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mhandisi Hamadi Masauni ameyasema hayo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Mh. Faharia Shomali aliehoji ni wahamiaji haramu wangapi wamekamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Amesema wahamiaji haramu 13,393 kati yao wahamiaji 2,815 walishitakiwa, 117 walitozwa faini, 429 walifungwa, 6316 waliondoshwa Nchini, 1353 waliachiwa huru baada ya kutoa nyaraka za uthibitisho wa uhamiaji wao na kesi zigine 2363 zinaendelea katika mahakama mbalimbali Nchini,

Amesema jitihada mbalimbali zimekuwa zikifanyika ili kuhakikisha wahamiaji haramu hao wanarudi Nchini mwao baada ya kumalizika kwa vifungo vyao zoezi ambalo hufanyika kwa kuratibiwa na Serikali kwa kushirikiana na taasisi ya uhamiaji Dunia IOM

Baada ya kukamilika kwa shughuli vikao vya bunge, waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Dokta Hussen Ally Mwinyi akimuwakilisha waziri mkuu amewaongoza wabunge katika zoezi la kuuaga mwili wa aliekuwa mbunge wa jimbo la buyungu wilayani kakonko marehemu Kasuku Samsoni Bilago ambapo amesema tukio hilo linawakumbusha wanadamu kuishi kwa kutenda mema wawapo duniani.

Mwili wa aliekuwa mbunge wa jimbo la Buyungu Wilayani Kakonko Mkoani Kigoma Marehemu Mwl. Kasuku Samson Bilago unatarajiwa kupumzishwa katika makao yake ya milele mapema hapo kesho Wilayani Kakonko .

Na Pius Jayunga                                            Bunge/Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...