Skip to main content

MWANASHERIA AISHAURI SERIKALI KUBADILISHA SHERIA YA NDOA YA MWAKA 1971


                         
Image result for SHERIA YA NDOA



Sheria ya ndoa ya mwaka 1971 ambayo inaeleza mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 14 hadi 18 kuolewa kwa ridhaa ya baba au mlezi wake imetajwa kuathiri zaidi watoto ambao wanaishi katika familia masikini na duni kutokana na kuolewa kwa umri mdogo. 

Akizungumza na DODOMA FM mwanaharakati wa haki za binadamu ambaye pia ni mwanasheria kutoka jijini Dar es Salaam bwana Jebra Kambole amesema kuna haja ya serikali kuibadilisha sheria hiyo kutokana na kuwa chanzo kisababishi cha ukatili wa kijinsia.

Amesema kitendo cha mtoto kuolewa akiwa na umri mdogo kutokana na sheria hiyo inavyoruhusu kuna athari kubwa kiafya ambapo amebainisha kuongezeka kwa idadi ya wanawake wenye FISTULA pamoja na maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI.

Hivi karibuni chama cha waandishi wa habari wanawake nchini TAMWA kiliandaa semina kwa vyombo vya habari mkoani Dodoma lengo ikiwa ni kuwapa ujuzi namna ya kuihamasisha serikali kufanya marekebisho katika sheria ya ndoa ya mwaka 1971.

Kwa mujibu wa sheria ya ndoa ya mwaka 1971 inaruhusu mwanamke kuolewa akiwa chini ya umri wa miaka 18. Kifungu cha 17 kinaeleza kwamba mwanamke ambaye hajatimiza miaka 18 anaweza kuolewa kwa idhini ya baba au kama baba amefariki basi mama na ikiwa wote wamefariki basi idhini hiyo yaweza kutolewa na mlezi wake.

BERNAD FILBERT                                                                      DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...