Skip to main content

MWAKA JANA YAMERIPOTIWA MATUKIO 41,416 YA UKATILI WA KIJINSIA

                          Image result for NAIBU WAZIRI WA AFYA NDUGULILE



Serikali imesema katika kipindi cha Januari hadi mwezi Desemba mwaka 2017 Jeshi la polisi Nchini limeripoti kupokea matukio yapatayo 41,416 ya vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto.

Naibu Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dr. Faustine Ndugulile ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali namba 49 la Mbunge wa viti maalumu Mwatumu Dau Haji aliehoji juu ya takwimu za matukio ya ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto.

Naibu Waziri wa Afya amesema kati ya matukio hayo, matukio 13,457 ni ya ukatili wa kijinsia kwa watoto kitendo ambacho Serikali imekuwa ikihakikisha inayatokomeza huku jamii ikitakiwa kutoa taarifa mapema katika vyombo vya sheria pale matukio hayo yanapojitokeza.

Kutokana na takwimu hizo Dr. Ndugulile amekiri kuongezeka kwa matukio ya ubakaji na ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto na katika kukabiliana na tatizo hilo Serikali kwa kushirikiana na wadau imechukua hatua mbalimbali ikiwemo kuzindua mpango wa Taifa wa miaka mitano wa mwaka 2017/18 hadi 2020/21/22 wa kutokomeza ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto.

Dr. Ndugulile amesema kutokana na mwitikio mkubwa wa wananchi kujitokeza kutoa taarifa za ukatili wa kijinsia kumechangiwa na ongezeko la ukubwa wa tatizo hilo na kutokana na changamoto hiyo Dr. Ndugulile amewataka wananchi kuacha utamaduni wa kutatua migogoro hiyo katika ngazi ya familia badala yake taarifa hizo zifikishwe moja kwa moja katika vyombo vya sheria.

Na Pius Jayunga                                                                  DODOMA  FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...