Skip to main content

MKUU WA MKOA WA DODOMA AMSIMAMISHA KAZI AFISA MANUNUZI KWA UBADHIRIFU.

                          Image result for RC BINILITH MAHENGE


Mkuu wa mkoa wa Dodoma DR. BINILITH MAHENGE amemsimamisha kazi aliyekuwa Afisa Manunuzi katika ujenzi wa majengo ya kituo cha Afya yanayoendelea kujengwa katika  Tarafa ya Mpwayungu wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma Bw.Ebby Mwakajila Kwa matumizi mabaya ya  pesa za ujenzi huo.

Tukio hilo limetokea baada ya Mkuu  wa mkoa kufanya ziara katika ujenzi huo wa majengo ya kituo cha Afya ambapo imegundulika kuwepo kwa upungufu wa fedha kiasi cha Tsh.milioni 3  ambazo zimetumika kinyume na utaratibu na kumtaka mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Chamwino kusimamia pesa hizo kurudi katika kazi yake.

Akizungumzia juu ya ubadilifu wa pesa hizo mkurugenzi wa wilaya ya Chamwino Bw. Athumani Masasi amekiri kuwepo kwa uzembe wa aliyekuwa afisa manunuzi wa awali ambapo alimwondoa katika sekta hiyo kabla ya mkuu wa mkoa kumsimamisha kazi na kumuweka mwingine hadi uchunguzi utakapomalizika.

Pamoja na hayo kamati ya ujenzi wa kituo cha Afya Mpwayungu wakiwakilishwa na mjumbe wao Bw.Amani Samweli Mazengo wamesema kumekuwa na changamoto mbalimbali zinazowaikabili ikiwemo kupishana kwa mahesabu kati ya mzabuni na kamati ya ujenzi.

Mbunge wa jimbo la Mtera Mh.Livingstone  Lusinde pamoja na mkuu wa wilaya ya chamwino Mh.Vumilia Nyamonga wameishukuru serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kutoa pesa kwa ajili ya unjenzi wa vituo vya Afya mbalimbali nchini.


Na ANIPHA RAMADHANI                                    CHANZO :DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...