Skip to main content

MKAKATI WA SERIKALI JUU YA UUZAJI WA CHAKULA NJE YA NCHI


Image result for BALOZI AUGUSTINE MAHIGA





Serikli imesema ina mkakati wa kuhakikisha kunakuwepo na akiba ya kutosha ya mazao ya chakula ikiwemo zao la mahindi na baada ya hapo hakutakuwa na kizuizi cha kuuza mazao hayo nje ya nchi.

Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Agustine Mahiga ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Temeke Abdalah Mtolea aliehoji Serikali ina mpango gani kuruhusu uuzwaji wa mazao ya mahindi nje ya nchi ili kuruhusu wananchi kufaidika na fursa zilizopo katika soko la Afrika ya Mashariki.

Amesema dhamira ya Serikali ni kuhakikisha hakuna changamoto ya upungufu wa chakula Nchini na hasa zao la mahindi na kinachofanyika kwa sasa ni kujengwa maghara ya kuhifadhia mazao hayo pamoja na kufanya tathimini ya kutosha ili kuona kiwango cha zao la mahindi kilichopo Nchini iwapo kinatosheleza kisha itaruhusu akiba ya mazao hayo  kuuza nje ya nchi.

Akielezea njia zinazotumika kutangaza fursa zilizopo katika jumuiya ya Afrika Mashariki Balozi Mahiga amesema hakuna njia tofauti ya kuwafikishia wananchi fursa zilizopo kinyume na zile ambazo zimekuwa zikitumika ikiwemo njia ya Redio, Television, pamoja na kufanya makongamano katika maeneo ya Vijijini hatua iliyoleta mafanikio makubwa.

Katika hatua nyingine Balozi Mahiga amesema tangu kuanzishwa kwa Bunge la Afrika Mashariki mwezi nov. 2001 hadi sasa jumla ya sheria 78 zimekwisha kutungwa na sheria 20 zimekwisha kuridhiwa na wakuu wa Nchi wanachama wakati sheria zingine zikiwa katika hatua mbalibali za kuridhiwa na kusainiwa, huku sheria zilizotungwa zikiwa zimelenga kuimarisha biashara, kukuza uchumi wa Nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Na Pius Jayunga                                                  Bunge/Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...