Skip to main content

MIPANGO YA SERIKALI KUFIKISHIA WAKULIMA PEMBEJEO KWA WAKATI

                             Image result for Naibu Waziri wa kilimo Dr. Merry Mwanjelwa




Serikali imesema zoezi la usambazaji wa pembejeo za kilimo linafanywa na sekta binafisi Nchini yakiwemo makampuni katika kuifikishia jamii hudumu ya pembejeo za kilimo na jukumu la Serikali ni kuratibu mahitaji, upatikanaji na matumizi yake.

Naibu Waziri wa kilimo Dr. Merry Mwanjelwa ameyasema hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mpanda Mjini Mh. Sebastian Simon Kapufi aliehoji ni lini Serikali itahakikisha inasambaza pembejeo kwa wakati na kwa kuzingatia msimu wa jiografia na maeneo husika.

Amesema pamoja na majukumu hayo bado Serikali inaendelea kuandaa mifumo ya kuhakikisha pembejeo za kilimo  zinasambazwa na kuwafikia wakulima wengi  kwa bei nafuu zaidi na ili kutekeleza azima hiyo 2017/18 Serikali ilianza kutumia mfumo wa ununuzi wa mbolea kwa pamoja na kuhakikisha mbolea hiyo inapatikana na kusambazwa kwa wananchi.

Amesema mfumo huo umeleta faida kubwa ikiwemo kuongezeka kwa upatikanaji wa pembejeo za kutosha kutoka tani 277,935 kwa mwaka 2016/17 hadi tani 310,673.7 mwezi april na kuchangia kupungua kwa bei ya mbolea kati ya asilimia 11 hadi 39.5 ikilinganishwa na bei ya mbolea hiyo kabla ya mfumo wa ununuzi wa mbolea kwa pamoja.

Aidha amesema Serikali imejipanga kuongeza uzalishaji wa mazao na teknolojia ya hali ya juu lengo kubwa ikiwa ni kuwawezesha wakulima kuendesha kilimo chenye tija na kufanikisha upatikanaji wa mazao ya kutosha ili kukidhi mahitaji katika soko la mazao hayo.

NA PIUS JAYUNGA                                                    DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...