Skip to main content

MAVUNDE ASEMA MFUMO WA VYAMA VINGI UMEPANUA WIGO WA DEMOKRASIA


Image result for WAZIRI MAVUNDE




Naibu waziri ofisi ya Waziri mkuu Sera, Bunge, Kazi Ajira na wenye ulemavu Mh. Athony Peter Mavunde amesema tangu kuanza kutumika kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa Nchini kumekuwa na mafanikio mengi ikiwemo kupanuka kwa wigo wa demokrasia ya vyama vingi vipatavo 19.

Mh. Mavunde ameyasema hayo leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Kiwani Abdalha Haji Ally alietaka kufahamu ni faida zipi pamoja na changamoto zilizo jitokeza Nchini baada ya miongo miwili na nusu ya kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi.

Amesema mfumo wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa umekuwa na faida pamoja na changamoto zake ikiwemo ongezeko la uhuru wa kuchagua viongozi wa vyama vya siasa walio nadi sera zao, kuongeza uwajibikaji kwa Serikali huku changamoto zilizo jitokeza ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa gharama za kuendesha gharama za kisiasa katika ngazi mbalimbali za uchaguzi.

Akifafanua juu ya uendeshaji wa mikutano ya kisiasa Nchini, Mh. Mavunde amesema si kweli kuwa Serikali imezuia harakati za kisiasa na badala yake umewekwa utaratibu maalumu wa kuendesha siasa kutokana na sheria mbalimbali za Nchi huku akiweka wazi sheria ya vyama vya siasa sura  258 imempa mamlaka msajili kuhakikisha anavilea vyama vya siasa na kusaidia vyama hivyo katika utatuzi wa migogoro.

Katika hatua nyingine Mh. Mavunde amesema lengo la Serikali ni kuendelea kukuza demokrasia ndani ya Nchi na makubaliano ya mwaka 2002 ya kuanzisha chuo cha mafunzo kwa wanasiasa yataendelea kufatiliwa ili kujenga Taifa la watu wenye uzalendo na nia ya kutumikia watanzania kupitia chuo kitakachokuwa na jukumu la kuoka wanasiasa.

Na Pius Jayunga                                                        Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...