Skip to main content

MAHAKAMA YAONDOA SHAURI LA KUPINGA MAUDHUI YA MTANDAO








Mahakama Kuu ya Mtwara imeondoa mahakamani shauri la kupinga  matumizi ya Kanuni za Maudhui ya Kimtandao (Online Content Regulation) lililofunguliwa na Kituo cha Sheria na  Haki za Binadamu (LHRC) na wenzake dhidi ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

Mbali na LHRC wengine waliopeleka zuio hilo ni Tanzania Human Rights Defenders (THRD); Baraza la Habari Tanzania(MCT) na Jamii Media; Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA ); na Jukwaa la Wahariri (TEF).

Kanuni hizo zilipaswa zianze kutumika Mei 5 lakini mahakama hiyo ikaweka zuio la muda Mei 4, baada ya kuwasilishwa kwa shauri la kupinga mahakamani hapo.

Kesi hiyo namba 12/2018 ilisomwa jana Mei 28 mbele ya Jaji Mfawidhi, Dk Fauz Twaib na ilipangwa kutolewa  uamuzi juu ya mapingamizi matatu yaliyowasilishwa na upande wa Serikali.

Akitoa uamuzi huo jana, Jaji Dk Twaib alisema mahakama hiyo imekubali pingamizi moja kati ya matatu yaliyowasilishwa; kwamba mashirika yaliyopeleka kesi mahakamani hapo hayana maslahi ya kutosha kwa maana ya kufungua shauri hilo na kwamba hawakuonyesha  namna moja kwa moja yatakavyoguswa na kanuni hizo.

Hivyo, mahakama iliondoa shauri hilo lakini inatoa nafasi kwa mashirika hayo kama yatahitaji kupeleka shauri lingine kama watajidhihirisha wana nafasi ya kufanya hivyo.

Na Zania Miraji

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...