Skip to main content

KATAZO LA RAIS KUTORUHUSU MWANAFUNZI ALIEPATA MIMBA KUENDELEA NA MASOMO LIPO KWA MUJIBU WA SHERIA

                                          Image result for NAIBU WAZIRI WA ELIMU OLE NASHA




Naibu Waziri wa elimu sayansi na teknolojia Mh. William Tate Ole Nasha amesema katazo la wanafunzi waliobebeshwa ujauzito kutokurudi shuleni lipo kwa mujibu wa sheria na Rais ameshalitolea msisitizo.

Mh. Ole Nasha ameyasema hayo leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge Suzan Limo alietaka kujua Serikali imeshafanya tathimini kuona ni athari gani za kijamii, kiuchumi pamoja na kisaikolojia kwa watoto wanaozaliwa na mabinti hao ambao ni wanafunzi.

Amesema katazo hilo limekuwepo tangu mwaka 2002 kwa mujibu wa kanuni iliyoanzishwa kipengele cha 60, ya sheria ya elimu ya mwaka 1978 na maelekezo yaliyotolewa na Rais Dr. John Pombe Magufuli hivi karibuni ya wanafunzi hao kutokurudi shuleni ni kusisitiza juu ya katazo hilo.

Naibu Waziri Ole Nasha amesema Serikali imechukua uamzi huo ili kumlinda mwanafunzi aliebebeshwa ujauzito kuepuka kunyanyaswa na wanafunzi wengine kutokana na hali aliyo nayo sambamba na kuonesha ni jinsi gani Serikali haiwezi kuendelea kuhudumia mwanafunzi aliebebeshwa ujauzito.

Aidha amesema Serikali inatambua tatizo la wanafunzi hao kubebeshwa mimba wakiwa masomoni kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo zile wasizoweza kuzihimili kama kubakwa, kutembea umbali mrefu kwenda shule, mila na desturi potofu pamoja na kukosekana kwa mahitaji ya msingi kutoka kwa wazazi na kwamba Serikali imeanza mikakati mbalimbali ya kutatua changamoto hizo.

Na Pius Jayunga                                           Bunge/Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...