Skip to main content

JAMII YAASWA KUIJUA SHERIA YA UKIMWI KUTAMBUA HAKI ZAO

Image result for SHERIA YA UKIMWI







Watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI wametakiwa kuifahamu sheria ya UKIMWI ili kuzitambua haki zao za msingi ambazo mara nyingi zimekuwa zikikiukwa.

Hayo yamebainishwa na Afisa sheria kutoka Tume ya kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACADS) Bwana Miraji Mambo wakati akitoa ufafanuzi wa sheria ya ukimwi katika mkutano uliofanyika jijini Dodoma wa  ukihusisha Konga za watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI.

Amesema haki nyingi za watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI zimekuwa zikikiukwa ikiwemo haki za  kutibiwa na haki za kutobaguliwa huku akilitaka jeshi la polisi na mahakama kuifahamu sheria  hiyo ili waweze kutekeleza matakwa ya sheria hiyo.

Mapema akifungua kikao hicho cha kuzijengea uwezo Konga za watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi,  Kaimu mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya kudhibiti Ukimwi Tanzania TACADS Bwana Jumanne Isango amesema mapambano dhidi ya Ukimwi ni hatua endelevu katika kuhakikisha watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi wanakuwa kwenye uangalizi na kwamba sheria ya Ukimwi ni muhimu katumika ili kulinda haki zao.

Ameongeza kuwa ili kufikia malengo ya mwaka 2030 ya kutokuwa na maambukizi ya ukimwi jamii inatakiwa kushishirikiana katika nyanja zote bila kubagua jinsia wala kabila.

Mkutano huo wa siku moja umehusisha Konga za watu wanaoishi na virusi vya ukimwi kutoka halmashauri za wilaya zote za mkoa wa Dodoma, Singida,Shinyanga na Tabora wakiwemo wawakilishi wa polisi kutoka iringa , Tabora, Dodoma , Singida na Dar es Salaam.

Na ANIPHA RAMADHAN                                         DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...