Skip to main content

HUDDERSFIELD TOWN YASALIA LIGI KUU

Alama moja katika uwanja wa Stamford Bridge umeihakikishia klabu ya Huddersfield kuwepo katika ligi kuu nchini Uingereza katika msimu ujao, matokeo ya leo yanawafanya kufikisha alama 37 katika msimamo wa ligi alama ambazo zinawahakikishia uwepo katika ligi kuu.

Habari nyingine kubwa katika mchezo wa leo ni namna ambavyo kocha wa Chelsea Antonio Conte alikipanga kikosi chake akimuacha Eden Hazard nje pamoja na Olivier Giroud na alama moja waliyoipata hii leo inawaweka katika hatihati kushiriki Champions League msimu ujao.

Suluhu ya leo ya Huddersfield inamaanisha kwamba timu zote zilizopanda daraja msimu huu zinabaki ligi kuu na hii ikiwa ni mara ya tatu katika historia ya Epl kwa jambo kama hili kutokea ambapo ilishatokea msimu wa 2001/2002(Blackburn, Fulham na Bolton) na ikatokea pia 2011/2012(Swansea, Norwich na Qpr).

Kwingineko mabao mawili ya Riyad Mahrez na moja la Jamie Vardy yalitosha kuiua Arsenal bao 3 kwa 1, ambapo matokeo haya yanawafanya Arsenal kuwa timu ambayo inaongoza kwa matokeo mabovu ugenini kuliko timu yeyote katika ligi kuu 5 kubwa barani Ulaya kwa mwaka 2018.

Manchester City waliipiga Brighton & Hove Albion mabao 3 na hii kuwafanya City kushinda michezo 31 katika msimu huu wakiifikia rekodi ya Tottenham waliyoiweka 1960/1961 ya kushinda idadi ya michezo kama hiyo katika ligi, lakini pia Gurdiola anakuwa ameivunja rekodi ya Jose Mourinho ya kumaliza ligi akiwa na alama nyingi ambapo Pep amefikisha 97, huku Mou alifikisha 95 msimu wa 2004/2005.

 

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...