Skip to main content

HATI MILIKI MIA NNE KUTOLEWA KATIKA VIJIJI 30 NCHINI

                                     Image result for SHIRIKA LA PELUM TANZANIA WILAYA BAHI




Zaidi ya hati miliki Elfu nne (4000) za kimila zinazohusisha umiliki wa ardhi zinatarajiwa kutolewa  na shirika la Pelum Tanzania katika vijiji 30 nchini.

Maeneo yatakayohusika na hati hizo ni  Wilaya za Mvomero, Morogoro, Kilolo, Mufindi, Bahi pamoja na Kongwa ili kufanikisha mpango wa matumizi bora ya ardhi vijijini.

Hayo yamebainishwa leo na afisa mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Kusimamia Sekta ya ardhi na Kilimo, kutoka shirika la PELUM TANZANIA Bi Anna Marwa wakati akizungumza katika mdahalo maalumu wilayani Bahi Mkoani Dodoma  uliowakutanisha viongozi mbalimbali wakiwemo madiwani na wenyeviti wa vijiji wenye lengo la kutambua usimamizi wa mpango wa matumizi sahihi ya ardhi.

Amesema kuwa June Mwaka huu Mradi huo unatarajia kufikia tamati, na unamalizika ukiwa umeacha mabadiliko makubwa katika vijiji 30 vya wilaya hizo ambapo mbali na kutoa hati miliki kwa wananchi hao mradi huo umeweza kutatua migogoro ya ardhi kwa kiasi kikubwa huku asilimia 30 ukiwasaidia wananchi kunufaika na uelewa juu ya masuala ya ardhi.

Awali akifungua mdahalo huo mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Bahi ambaye ni diwani wa kata ya Mwitikia Bwana Danford Chisomi amewataka wananchi kutumia mafunzo hayo kujiletea maendeleo kupitia fursa ya umiliki wa ardhi huku akiwataka wenyeviti wa vijiji kusimamia kikamilifu majukumu yao ikiwa ni pamoja na kuendelea kutatua migogoro ya ardhi ili kufikia malengo mahususi yaliyokusudiwa.

Nao baadhi ya wananchi walionufaika na mradi huo wamelishukuru shirika hilo kwa kutoa mafunzo hayo na kuahidi kuwa chachu ya kuleta maendeleo katika jamii kwa kutoa mafunzo kwa wananchi wengine ili kukomesha migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ni tatizo kubwa hapa nchini.

Mnamo mwaka 2013 Shirika la PELUM TANZANIA kupitia Ufadhili wa Shirika la Misaada la Watu wa Marekani, lilianzisha mradi wa Ushiriki wa Wananchi katika Kusimimia Sekta ya Kilimo, unaojulikana kama CEGO (CITIZEN ENGANGING IN GOVERNMENT OVERSIGHT) mradi ambao umetekelezwa katika mikoa Mitatu ya Morogoro, Iringa na Dodoma na unatarajia kufikia kikomo ifikapo june 9 mwaka huu.

 Na Alfred Bulahya.                                                       Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...