Skip to main content

HALMASHAURI YATEGEMEA HISANI YA WADAU KUENDELEZA MIRADI YA MAENDELEO


Image result for WILAYA YA KONGWA DODOMA







Ukosefu wa fedha kutoka kwa wahisani na wadau mbalimbali imetajwa kuwa chanzo kikubwa kinachopelekea  kushindwa kukamilika kwa miradi mbalimbali ya maendeleo katika wilayani ya Kongwa Mkoani Dodoma.

Hayo yamebainishwa na kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kongwa  Dkt Omary Nkhullo wakati akiwasilisha taarifa ya miradi ya maendeleo katika kipindi cha robo tatu ya mwaka wa fedha 2017/2018 kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Kongwa.

Amesema kuwa katika robo ya tatu ya mwaka kuanzia mwezi Januari hadi Machi mwaka huu halmashauri ilitegemea kupokea kiasi cha shilingi Bilioni Moja Milioni Mia sita ishirini na tano  laki mbili na elfu ishirini na tisa kutoka katika ruzuku ya maendeleo lakini hadi kufikia mwisho wa robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2017/2018 halmashauri haijapokea pesa hizo.

Ameongeza kuwa katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka wa fedha 2017/2018 halmashauri imepokea kiasi cha shilingi bilioni Moja Milioni Mia mbili sabini na nane laki tatu elfu sitini na 2 mia sita sitini na nane.(1,278,362,668) pekee kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kongwa ambaye pia ni diwani wa kata ya Kongwa White Zubery amewataka madiwani wote kuhakikisha wanasimamia fedha zinazopatikana katika kata zao kupitia makusanyo mbalimbali ili kuendelea kukuza uchumi wilayani humo.

NA ALFRED BULAHYA               CHANZO :DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...