Skip to main content

HALMASHAURI YATAKIWA KUTEKELEZA KWA VITENDO USIMAMIAJI WA ARDHI

                                    Image result for MIGOGORO YA ARDHI WILAYA YA BAHI






Halmashauri ya wilaya ya Bahi mkoani Dodoma imetakiwa kusimamia kikamilifu mpango wa matumizi sahihi ya ardhi wilayani humo kwa kuhakikisha kila mmoja anatekeleza majukumu yake katika kuleta maendeleo ya nchi.

Wito huo umetolewa mapema wiki hii na BwanaPraygod Shao wakati akizungumza na taswira ya habari kwa niaba ya Kamishina Mkuu Wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi ambapo amesema kuwa licha ya serikali kutumia gharama nyingi kusimamia jambo hilo bado kuna changamoto ya baadhi ya viongozi kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo hali inayochangia kuendelea kuwepo kwa migogoro ya ardhi katika maeneo mbalimbali.

Amesema kuwa changamoto kubwa inayosababisha migogoro mingi ya ardhi ni suala la upimaji kutotiliwa mkazo na kuwataka wahusika kama mabaraza ya ardhi kusimamia kikamilifu suala hilo kwa kutumia kanuni na taratibu pamoja na kuwamilikisha wahusika viwanja vyao baada ya kuvipima ili wanufaike na umiliki huo kama kupewa mikopo na sekta za kifedha pindi wanapohitaji.

Aidha amewataka wananchi kuacha kukimbilia katika ngazi za juu kutafuta suluhu wanapokumbana na migogoro na badala yake waanzie katika ngazi za chini kwani ndiko mahali sahihi suala la ardhi linakoanza kusimamiwa huku akiyataka mabaraza kusuluhisha migogoro na sio kutoa maamuzi ya kesi.

Na Alfred Bulahya                                              DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...