Skip to main content

CHANGAMOTO ZINAZOKWAMISHA KUKUA KWA UCHUMI WA VIWANDA

Changamoto ya ukosefu wa wawekezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo katika viwanda, kilimo na miundo mbinu ni chanzo cha kushindwa kukua kwa uchumi wa viwanda na maendeleo ya watu hapa nchini.


Hayo yamebainishwa leo mjini Dodoma na Gavana wa benki kuu ya Tanzania BOT Prof, Florence Luoga wakati akifungua warsha ya wadau wa sekta ya fedha nchini iliyolenga kujadili mchango wa sekta ya fedha kwenye maendeleo ya uchumi.

Akisoma hotuba hiyo kwa niaba ya waziri wa fedha na mipango Dkt Philpo Mpango prof Luoga amesema kuwa changamoto hizo ikiwa ni pamoja na wananchi wengi kutofikiwa na huduma za fedha zimechangia mchango wa fedha na bima kwenye pato la taifa ndani ya miaka 5 iliyopita kuendelea kubaki asilimia 3.5 kiasi ambacho si cha kuridhisha.

Aidha katika kukabilia na changamoto hizo amewataka wadau mbalimbali katika sekta ya fedha ikiwemo sekta ndogo ya benki na bima kuhakikisha wanaboresha  huduma kwa wateja ili kuweza kupata faida itakayowawezesha kulipa kodi na kuongeza wigo wa upatikanaji wa bima za kilimo hali ambayo itasaidia kuchangia maendeleo ya taifa.

Awali akisoma hotuba ya katibu mkuu wizara ya fedha naibu katibu mkuu Dkt Khatibu Kazungu amesema kuwa kwa mujibu wa utafiti wa shirika la FINCECOP wa  mwaka 2017 unaonyesha kiwango cha matumizi ya fedha kinaongezeka kutokana na kuwepo kwa ubunifu katika utoaji wa huduma ambapo tangu sekta ya fedha ilipoanzisha huduma ya fedha kupitia simu za mikononi mwaka 2009 mpaka sasa imefikia asilimia 65 kutoka asilimia 15.9

Serikali inaendelea kufanya maboresho katika sekta ya fedha kwa lengo la kutatua changamoto mbalimbali na kuweka misingi imara ya kuwezesha ukuaji , ushindani, na ufanisi katika sekta ya fedha.

Na Alfred Bulahya 


Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...