Skip to main content

AVULIWA UKATIBU KWA TUHMA ZA KUNYANYASA WAFANYAKAZI KWA KAULI CHAFU

             Image result for MKURUGENZI wa halmashauri ya Chamwino Jijini Dodoma ATHUMAN MASASI                     



MKURUGENZI wa halmashauri ya Chamwino Jijini Dodoma ATHUMAN MASASI amemvua   madaraka ya ukatibu ndugu EKIA SHUMA katika hospitali  ya Wilaya hiyo  kwa tuhuma za unyanyasaji dhidi ya wafanyakazi.
Mkurugenzi amefikia hatua hiyo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wafanyakazi wa hospitali hiyo wakimtuhumu katibu huyo kuwanyanyasa watumishi,Kwa kutoa majibu kwa namna anavyotaka na kutosikiliza shida za watumishi.
Akizungumza katika kikao cha wafanyakazi baada ya kusikiliza malalamiko na kero za watumishi mkurugenzi MASASI ametoa onyo pia kwa mlezi wa watumishi wa kike(MATRONI)NEEMA MLULA kutokana na kulalamikiwa pia kuwanyanyasa watumishi.
Katika hatua nyingine ameuagiza uongozi wa hospitali kujibu hoja 12 zilizotolewa na mkaguzi wa hesabu za ndani wa halmashauri NGERANGERA TELESPHORD ambapo jumla ya shilingi milioni 608.7 zimetumika bila ya kuwa na viambatanisho na hazikufuata mfumo wa manunuzi ya umma.
Awali mkaguzi TELESPHORD amewasilisha baadhi ya hoja zilizoanzia mwaka 2014 hadi machi mwaka 2017.
Katika kikao hicho mkurugenzi huyo amesikiliza  kero na matatizo ya watumishi hao ambapo wengi walilalamikia kutolipwa mishahara na DCT,kutopandishwa vyeo kwa wakati jambo ambalo aliahidi kulifuatilia ili kutatua changamoto hizo ikiwemo mtumishi mmoja aliyelalamikia kunyimwa ruhusa ya kwenda masomoni ilihali alikuwa na ufadhili suala ambalo mkurugenzi alimtaka katibu wa hospitali kulitolea ufafanuzi jambo hilo.
NA,MINDI JOSEPH                                                           DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...