
Vyombo vya habari
kote nchini vimeombwa kutoa ushirikiano katika utoaji wa elimu kwa wananchi juu
ya uvaaji wa mavazi yenye maadili ili kujenga utamaduni bora wa nchi yetu.
Rai hiyo imetolewa na Afisa Utamaduni wa halmashauri ya jiji la Dodoma Bw.Desdery Kunzinza wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya hali ya uvaaji kwa kuzingatia maadili ya Kitanzania.
Amesema vyombo vya habari
vina nafasi kubwa katika kuhabarisha, kukosoa na kuionya jamii juu ya uadilifu wa uvaaji wa mavazi
unaoendelea kujitokeza katika maeneo mbalimbali.
Bwana Desdery amesema
kuwa jukumu la kujiheshimu linamlenga mtu mwenyewe hivyo ni vyema kujiheshimu
kwa kuzingatia kanuni bora za uvaaji ili kuondokana na mvutano kati ya wanaokiuka maadili ya uvaaji na sheria inayo wabana.
Amesema kanuni
zilizopo zinawabana watumishi wa UMMA pekee na hakuna kanuni zozozote
zilizowekwa kwa ajili ya kuibana jamii kiujumla .
Aidha Bwana Desdery amewashauri wamiliki wa kumbi za starehe kutowabana wafanyakazi wao kwa
kuwataka kuvaa mavazi ambayo yatawavutia wateja wengi kwani wanachangia
kuporomosha maadili.
Na
ANIPHA RAMADHANI DODOMA FM
Comments
Post a Comment