Skip to main content

ZAIDI YA MILIONI 60 ZIMELIPWA NA MAHAKAMA KAMA FIDIA KWA MASHAURI 16

                             Image result for Waziri Palamagamba


Jumla ya shilingi milioni 60,152,487.65 zimelipwa na mahakama kama fidia kwa mashauri 16 yaliyo hakikiwa na kuthibitishwa na mahakama baada ya kupokea fedha kutoka hazina kwa mwaka wa fedha 2015/16 hadi 2016/17.

Waziri wa katiba na sheria Prof Paramagamba Kabudi ameyasema hayo leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Jimbo la Rombo Mh. Joseph Selasini alietaka kufahamu iwapo Serikali inazikumbuku za taarifa za watu waliotozwa faini na kutakiwa kurejeshewa faini hizo.

Waziri Kabudi amesema madai 24 yenye jumla ya shilingi milioni 87 yameshachambuliwa na kufikishwa hazina tayari kwa kusubiri malipo wakati huohuo jumla ya madai 12 yenye thamani ya shilingi laki 9 yakiwa yamewasilishwa hazina tayari kwa malipo.

Waziri Kabudi amesema taarifa zote za wananchi wanaolipa faini zinatunzwa na mahakama na hivyo urejeshwaji wa fedha hizo hutegemea upatikanaji wa nyaraka zinazo thibitisha malipo ya faini kupokelewa na uwepo wa nakala ya hukumu.

Mh. Kabudi amesema wapo baadhi ya wananchi wasiotambua haki yao ya kurejeshewa faini ya fedha wanazotozwa baada ya kushinda kesi na hivyo ipo haja ya kutoa elimu ili kutambua haki hiyo.

Na Pius Jayunga                                               Chanzo: Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...