Skip to main content

ZAIDI YA DOLA 149.5 ZINAHITAJIKA KATIKA UJENZI WA MRADI WA KUFUA UMEME MTO MALAGARASI

              Image result for mradi wa kufua umeme kupitia mto Malagarasi


Zaidi ya dola mil. 149.5 zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa mradi wa kufua umeme kupitia mto Malagarasi Ibamba two uliopo katika Mkoa wa Kigoma.

Waziri wa Nishati Dr. Medard Kaleman ameyasema hayo leo bungeni mjini dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe aliehoji Serikali imefikia wapi katika utekelezaji wa mradi wa umeme wa maji katika mto Malagarasi ambao ndio suluhisho kwa Mkoa wa Kigoma.

Dr. Kalemani amesema mradi huo ulipangwa kutekelezwa mapema mwaka 2008 lakini ukashindwa kutekelezwa kutokana na sababu mbalimbali na tayari mradi huo umeingizwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/19 ambapo utekelezaji wake unatarajiwa kuanza.

Akizungumzia tatizo la kukatika kwa umeme Waziri Kalemani amesema tatizo hilo linatokana na kasoro ndogo ndogo ambazo zimekuwa zikijitokeza na tayari ufuatiliaji umekuwa ukifanyika katika maeneo yanayobainika kuwa na tatizo la kukatika kwa umeme.

Katika hatua nyingine naibu waziri wa nishati mh. Subira Mgalu amesema serikali kupitia mradi wa urban eletification itaendelea kuyafikishia huduma ya nishati ya umeme maeneo yaliyopo katika mamlaka za miji, manispaa pamoja na majiji.

Na Pius Jayunga                                                 Chanzo: Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...