Skip to main content

WAZIRI MKUU AWASILISHA BAJETI YA MAKADIRIO YA OFISI YAKE NA OFISI YA BUNGE KWA MWAKA WA FEDHA 2018/2019

                                                             Image result for WAZIRI MKUU KASIMU MAJALIWA


Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Kasimu Majaliwa ameliomba Bunge kuridhia na kuidhinisha fedha kiasi cha shilingi. Bil 124,958,230,698 kwa ajili ya makadilio ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu na ofisi ya Bunge kwa mwaka wa fedha 2018/19.

Waziri Mkuu  amewasilisha leo makadirio ya mapato na matumizi ya fedha ya ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge, kwa mwaka wa fedha 2018/2019 katika mkutano wa bunge la bajeti unaoendelea hapa mjini Dodoma.

Amesema kati ya fedha hizo bil. 66,162,789,698 zitaelekezwa katika matumizi ya kawaida na bil. 58,791,841,000 zitaelekezwa katika matumizi ya maendeleo huku akiliomba Bunge hilo kuidhinisha fedha kiasi cha sh. 125,521,100,000 kwa ajili ya mfuko wa Bunge.

Akielezea mafanikio yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dr. John Pombe Magufuli katika kipindi cha miaka miwili iliyopita waziri mkuu  Kasimu Majaliwa amesema serikali imefanikiwa kujenga nchi yenye uchumi imara, kuimarisha ulinzi na usalama, kufufua shirika la ndege la Tanznaia  pamoja na kupambana na dawa za kulevya.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya bunge  ya katiba na sheria Mh. Mohamed Mchengelwa amesema mpango wa bajeti ya ofisi ya waziri mkuu mwaka wa fedha 2018/19 umeainisha maeneo 23 ya vipaumbele ikiwemo kujenga uwezo wa serikali kukabiliana na maafa.

NaPiusJayunga                                                                   Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...