Skip to main content

WATU MILIONI 600 HUUGUA NA ZAIDI YA WATU LAKI 4 HUPOTEZA MAISHA KILA MWAKA KUTOKANA NA CHAKULA KISISCHOKUWA SALAMA


                          Image result for magonjwa yatokanayo chakula kisicho kuwa salama

Takribani watu milioni mia sita duniani kila mwaka huugua magonjwa mbalimbali  huku wengine laki nne na elfu ishirini hupoteza maisha kutokana na kula chakula kisichokuwa salama.

Hayo yamebainishwa leo na kaimu mganga mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt Nassoro Mzee wakati akizungumza kwa niaba ya katibu tawala wa mkoa kwenye ufunguzi wa mafunzo maalumu kwa wataalamu wa afya kutoka katika halmashauri 9 za mkoa wa Dodoma yenge lengo la kuwawezesha wataalamu kuongeza uelewa katika kuandaa taarifa za magonjwa yatokanayo na chakula.

Dkt Mzee amesema kuwa madhara yatokanayo na chakula kama kuhara damu,homa ya matumbo na kipindupindu ,yamekuwa ni tatizo kubwa  dunia kwani yamekuwa yakisababisha kuzorotesha uchumi wa nchi na hupelekea vifo na athari kubwa kwa jamii kutokana na baadhi ya wagonjwa kushindwa kumudu gharama za matibabu.

Aidha ametaja sababu mbalimbali zinazochangia uwepo wa chakula kisicho kuwa salama kuwa ni pamoja na jamii kutozingatia kanuni za ubora za uzalishaji kuanzia ngazi za mashambani, usafirishaji ,usindikaji na utayarishaji wa chakula hivyo ni vyema jamii ikawa na uangalizi madhubuti ili kuepusha madhara yatokanayo na chakula.

Kwa upande wake Meneja mkuu wa mamlaka ya chakula na dawa TFDA kanda ya kati dkt Engelbert Bilashomoka amesema kuwa  mkoa wa Dodoma umeonekana kuwa na magonjwa mengi yatokanayo na chakula licha ya kuwepo kwa changamoto ya kutotumwa taarifa kwa mamlaka hiyo hivyo amewataka wataalamu kuhakikisha wanatoa taarifa ili kuendelea kupambana na tatizo hilo.

Mpango wa kukusanya magonjwa yatokanayo na chakula ulianzishwa hapa nchini mwaka 2008 kwa lengo kufanya ufatiliaji mapema ili kuhakikisha magonjwa haya yanatokomezwa na amewataka waandaaji wa vyakula katika maeneo mbalimbali kuzingatia kanuni na taratibu sahihi za uaandaaji wa vyakula kama kunawa mikono na sabuni baada ya kutoka chooni ,kabla ya kuaanda  na kabla ya kula chakula.

Na Alfred Bulahya                                                     Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...