Skip to main content

WANANCHI WATAKIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA MUDA MFUPI KUONDOA TATIZO LA AJIRA


Wakazi wa Jiji la Dodoma wameaswa kuacha kuilalamikia serikali kuwa imeshindwa kutoa ajira kwa vijana badala yake wajikite  kuwekeza katika masomo ya ufundi ya muda mfupi ili kupunguza tatizo hilo.

Wito huo umetolewa na mkuu wa chuo cha VETA Dodoma  Ramadhani Mataka wakati akizungumza na Dodoma FM kupitia kipindi cha Taswira ya habari juu ya namna ya kuondoa tatizo la ajira kwa vijana.

Bwana Mataka amesema kuwa baadhi ya watanzania wamekuwa wakilalamikia serikali kuwa haitoi ajira badala ya kujiongeza kusoma hata kozi fupi zitakazowawezesha kujipatia vipato.

Amesema kuwa wakati Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania DKT John Pombe Magufuli akisisitiza uwepo wa serikali ya viwanda ni lazima watu wahakikishe wanasoma mafunzo ya ufundi wa fani mbalimbali ili kuviwezesha viwanda kufanya kazi kwa ufanisi na sio kutegemea watu wa mataifa mengine waje kufanya kazi katika viwanda hivyo.

Ameongeza kuwa lengo na madhumuni ya kuanzishwa kwa vyuo vya VETA ni kutokana na kuwepo kwa changamoto ya upungufu wa ajira nchini na moja ya majukumu yake ni kuhakikisha vinatoa mafunzo ya ufundi ili kuwawezesha vijana wanaotoka vyuoni wawe na maarifa yatakayowasaidia kupata ajira katika maeneo mbalimbali au kujiajiri wenyewe.

Katika hatua nyingine bw Mataka amesema wakati serikali ikiendelea kuhamia Dodoma waalimu waliopata nafasi ya kutoa mafunzo kwa wanafunzi wa chuo cha VETA Dodoma wanatakiwa kuhakikisha wanatoa mafunzo yenye uwezo wa kuwasaidia wawapo mitaani kwani wengi wao ni watoto wanaotoka katika familia duni.

Na Alfred Bulahya                                                    Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...