Skip to main content

WANANCHI WASHAURIWA KUACHA NGONOZEMBE KUEPUKA MAGONJWA KAMA INI N.K

                                        Image result for jiji la dodoma

Wakazi wa Jiji la Dodoma wametakiwa kuachana na ngono zembe ili kuepukana na magonjwa yasababishwayo na ngono zisizo salama.


Akizungumza na Dodoma FM daktari MUZNA UJUDI kutoka hospitali ya rufaa mkoani hapa  amesema kwasasa magonjwa ya ngono yamekuwa yakiwakabili watu wengi hususani ugonjwa wa homa ya INI ambao umekuwa ukiwapata watu wengi kupitia ngonozembe.

Dokta MUZNA amesema mbali na kuwa ugonjwa huu unaambukizwa kwa njia ya ngonozembe pia mtu anaweza kuupata kwa kuongezewa damu ya mtu ambae tayari ana virusi vya ugonjwa huo (HEPATATICS B) pamoja na kuchangia vitu vya ncha kali kama vile sindano kwaajili ya matibabu.

Pia ameeleza dalili za mwanzo za ugonjwa wa homa ya ini kuwa ni kubadilika kwa rangi ya macho kutoka katika hali ya kawaida na kuwa na unjano,kupata maumivu ya tumbo, kukojoa mkojo wenye rangi ya njano iliyokolea pamoja na mwili kuwa mchovu.

Aidha imeonekana kuwa dalili za ugonjwa huu zinaweza kutoonekana kabisa kwa kipindi cha mwanzo unapoambukizwa na kuja kuibuka wakati ukiwa tayari umeharibu INI jambo ambalo limepelekea mganga huyo kuwataka wakazi wa DODOMA kujihadhali kwa kupima afya zao mapema.

Sanjari na hayo ameitaka jamii kuachana na ngonozembe badala yake watumie kinga pamoja na kuwa waaminifu kwa kuwa na mpenzi mmoja ili kuepukana na maambukizi ya magonjwa ambayo yanaweza kuepukika.

Na Anipha Ramadhan                                                  Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...