Skip to main content

WANANCHI WAHOFIA DAMPO BUBU KUWALETEA MAGONJWA WAOMBA LIONDOLEWE

                            Image result for DAMPO AREA A  DODOMA MJINI


Wananchi  wa mtaa wa Kisabuje uliopo  Area A  Manispaaa ya Dodoma wameiomba halmashauri ya manispaa ya Dodoma kuwahamishia  Dampo lililopo katikati ya makazi yao ambalo limekuwa likiwakera  kwa kipindi cha takribani miaka miwili.

Wakizungumza na Dodoma FM wakazi hao wamedai  kuwa Dampo hilo limekuwa changamoto kwao kutokana na harufu inayotokana na taka zinazotupwa hapo kukaa muda mrefu bila kupelekwa katika eneo husika.

Aidha wamedai kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kupata magonjwa ya mlipuko kwani wadudu wasambazao magonjwa hayo wanaweza kusafirisha uchafu kutoka katika taka hizo na kupeleka  katika vyombo wanavyotumia kwa matumizi yao.

Akijibu tuhma hizo Mwenyekiti wa mtaa huo Bw.UHURU CHIWARIGO  amesema tayari taarifa hiyo ameipeleka  manispaa  na kwa afisa afya ambapo hadi sasa anasubiri mwitikio kutoka kwa ili kuhamishia taka hizo katika eneo lililopo Dampo la Sokoine.

Bw. Chiwarigo amesema moja kati ya changamoto ambayo inawatatiza katika mtaa huo ni kutofika kwa wakati kwa  magari yanayobeba taka jambo ambalo linapelekea kuhifadhi taka kwa muda mrefu katika eneo hilo ambalo ni hatarishi kwa maisha ya wananchi.

Hata hivyo amewataka wananchi wake kuwa wavumilivu kwa kipindi hiki kifupi na kusema kuwa tayari zoezi hilo lipo kwenye mikakati ambapo wanasubiria halmashauri kuleta kijiko kwa ajili ya kuziondoa taka hizo.

Na ANIPHA RAMADHAN                                   CHANZO:DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...