Skip to main content

WANANCHI MJINI DODOMA WAONYWA KUUZA MAENEO BILA KUFUATA SHERIA NA KANUNI

                                                       
Image result for MJI WA DODOMA


Wananchi mkoani Dodoma wametakiwa kuacha tabia ya kuuziana maeneo bila kufuata utaratibu  kutoka kwa viongozi wanaohusika na kitengo hicho.

Wito huo umetolewa na Afisa Habari wa Halmashauri ya manispaa ya Dodoma Bw.RAMADHANI JUMA wakati akizungumza na Dodoma FM ambapo amesema tangu sarikali ilipohamishia shughuli zake mkoani hapa  kumekuwa na migogoro ya ardhi.

Bw. Ramadhani amesema halmashauri ya manispaa ya Dodoma ilikabidhiwa shuguli za aridhi rasmi  tangu ilipovunjwa mamlaka ya ustawishaji Makao makuu CDA  mwezi MEI mwaka jana  ambapo hadi sasa wamefanikiwa kwa wasatani kutatua migogoro ya ardhi kwa baadhi ya maeneo katika manispaa ya Dodoma.

Kwa kipindi hiki ambacho manispaa imekabidhiwa shughuli za aridhii TAKWIMU zinaonesha kuwepo kwa migogoro ya aridhi 982 Tangu may mwaka jana hadi february mwaka  huu  ambapo hadi sasa wametatua takribani migogoro 411 huku mingine 572 ikishughulikiwa katika ngazi tofauti.

Aidha ameongeza kuwa wananchi wamechukulia fursa ya serikali kuhamia mkoani hapa kama kigezo cha wao kujipatia kipato kupitia maeneo waliyo nayo kwa kuuziana wao pamoja na wageni wanaohamia bila kufuata kanuni.

Afisa habari huyo amewatoa hofu wananchi wa mkoa wa Dodoma kuwa wameweka mikakati ya  mipamgo miji ambayo itasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto za ardhi kwa wananchi.

Na ANIPHA RAMADHAN                            CHANZO:DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...