Skip to main content

WANAFUNZI WENYE ULEMAVU KUPATIWA WALIMU MAALUM

                 8726-Waziri-Kakunda.jpg



Halmashauri zote Nchini zimeagizwa kuwahamishia walimu walio na uwezo wa kufundisha wanafunzi walio na ulemavu wakiwemo walio na usonji katika shule zilizo na uhitaji hadi ifikapo mwezi Desemba mwaka huu.

Naibu Waziri wa TAMISEM Mh. Joseph Kakunda ametoa maagizo hayo leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa kuteuliwa Mh. Salma Rashid Kikwete aliehoji Serikali inawasaidiaje watoto wenye usonji wapate elimu, pamoja na idadi ya walimu wao iwapo wanatosheleza.

Mh. Kakunda amesema mpaka sasa kuna jumla ya wanafunzi 1416 walio na tatizo la usonji huku idadi ya walimu wao wakiwa 157 walioko katika shule 18 za msingi Nchini idadi ambayo ni ndogo kulingana na idadi ya wanafunzi walio na uhitaji maalumu.

Amesema mkakati wa Serikali ni kuwatambua watoto walio na tatizo la usonji Nchini kote ili kuwapatia haki ya elimu kama ilivyo kwa watoto wengine huku mtoto mmoja alie na usonji akihitaji kufundishwa na mwalimu mmoja lakini kutokana na upungufu wa walimu inalazimu mwalimu mmoja kufundisha idadi kubwa ya wanafunzi.

Kutokana na upungufu wa walimu walio bobea katika ufundishaji kwa wanafunzi walio na ulemavu Mbunge Suzan Lyimo ameshauri kutoa kipaumbele cha ajira kwa walimu walio hitimu mafunzo hayo wakiwemo waliosomea katika chuo cha viziwi kilichopo Mkoani Tabora huku Naibu Waziri Kkunda akiahidi kutoa kipaumbelea cha ajira kwa walimu hao.

Na Pius Jayunga                                           Chanzo: Dodoma FM


Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...