Skip to main content

WANAFUNZI WASOMEA CHINI YA MBUYU KWA KUKOSA MADARASA

Image result for WANAFUNZI WASOMEA CHINI YA MBUYU KWA KUKOSA MADARASA CHAMWINO

Uhaba wa vyumba vya madarasa ni miongoni mwa changamoto inayoikabili shule ya msingi Mapinduzi iliyopo Kijiji cha Nzali kata ya Chilonwa Wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma  hali inayopelekea   wanafunzi  kusomea chini ya mbuyu.


Hayo yamebainishwa na Mkuu wa shule hiyo Bi Subira Salimu Wakati  wadau wa shirika la ACTION AID walipotembela  shuleni hapo wakiwa katika   shughuli mbalimbali za kuelekea kilele cha maadhimisho ya juma la Elimu Duniani.

Amesema shule yake ina jumla ya wanafunzi 202  kuanzia darasa  la kwanza hadi la saba sawa  na wasichana  108 na wavulana  94 huku ikiwa na vyumba 4 vya madarasa  hali inayopeleka  darasa la pili kusomea chini ya mbuyu.

Aidha amesema uhaba wa matundu ya vyoo  pia ni changamoto inayowakabili wanafunzi hao, ambapo amedai shule ina matundu ya vyoo  sita kwa wanaume na wanawake hali inayopelea kusubiriana wakati wa kujisaidia.

Akizungumza katika hadhara hiyo Kaimu  Afisa Elimu Wilayani hapo Bi Amina Mussa amewataka  wazazi kuacha kuwashinikiza watoto wao kutofanya vizuri katika mitihani yao ya kuhitimu na kudai kuwa watoto wa kike wanahitaji kupata Elimu sawa na watoto wa kiume.

Naye Katibu wa Jukwaa la Wanawake na Wakulima wilayani hapo JUWACHA lilipo chini ya  Shirika lisilo la Kiserikali  la ACTION AID Sophia  Bhoke  amesema wao kama  JUWACHA  wamefanya tathimini ya pima kadi na matokeo katika sekta ya Elimu wamegundua uhaba wa walimu ni tatizo kubwa kwa baadhi ya shule.

Hata hivyo  wazazi wa wanafunzi akiwemo  Magrent Mtango amesema changamoto inayowakumba watoto wao ni  pamoja na uhaba wa vitabu huku  wanafunzi wakitaja changamoto wananzo kutana nazo pindi wawapo shuleni.

Madhamisho ya kilele cha Juma la  Elimu  Duniani hufanyika  aprili 27 kila mwaka.

Na Alfred Bulahya                                                 DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...