Skip to main content

WAKULIMA WASHAURIWA NJIA SAHIHI YA KUHIFADHI NAFAKA ZISIHARIBIKE

                 Image result for NAMNA BORA YA KUHIFADHI NAFAKA


Wakulima mkoani Dodoma wameshauriwa kuvuna mazao ya nafaka yakiwa katika hali ya kukomaa  ili kuyaepusha kushambuliwa na wadudu wajulikanao kama dumusi  pindi watakapo yahifadhi kwa ajili ya chakula.

Ushauri huo umetolewa na Afisa kilimo mkoani Dodoma Bw. Benard Abraham wakati akizungumza na Taswira ya Habari ambapo amesema kuwa kwa kipindi hiki ambacho wakulima wanaelekea kuvuna ni vema wakatumia njia salama za uhifadhi wa mazao ili kuhakikisha yanakaa kwa muda mrefu bila kubunguliwa na wadudu.

Bw. Abraham amesema miongoni mwa sababu inayofanya mazao ya nafaka kukaa kwa muda mrefu bila kuharibika ni kuhakikisha yanakauka vizuri na kuondokana na hali ya unyevunyevu na kuhifadhi  katika mifuko ,maghala pamoja na vihenge.

Aidha amewataka wananchi kutotumia dawa kama njia ya kuzuia wadudu wanao haribu mazao kutokana na dawa hizo kuwa na madhara ikiwa zitatumika kinyume na taratibu  badala yake watumie njia salama ambayo ni mifuko, maghala pamoja na vihenge.

Pamoja na hayo Afisa Kilimo huyo amewataka wakulima kufuatilia mashamba yao na kutopuuzia pale wanapoona kuna dosari katika mimea ikiwa ni kuondokana na dhana ya kuwalalamikia maafisa ugani kuwa hawawatembelei katika mashamba yao na badala yake watoe ushirikiano kwa maafisa ugani wao.

Na ANIPHA RAMADHAN                               DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...