Skip to main content

WAGONJWA WA MALARIA KUTIBIWA BURE

                                                 Image result for MAADHIMISHO YA MALARIA


Wakazi wa Manispaa ya Dodoma wameshauriwa kuzingatia ushauri wa wataalamu wa afya wanaopewa ili kujikinga na ugonjwa wa malaria.

Rai hiyo imetolewa leo na Daktari wa zahanati iliyopo chini ya chama cha uzazi na malezi bora Tanzania (UMATI) iliyopo kata ya chamwino manispaa ya Dodoma Daktari JORAM ELIKANA wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya namna bora ya kudhibiti ugonjwa wa malaria.

Daktari Joram amesema kuwa kama jamii itazingatia ushauri na maelekezo kutoka kwa wataalamu wa afya kwa kutumia vyandarua wakati wa kulala na usafi wa mazingira ni dhahili kuwa  ugonjwa wa maralia utapungua kama sio kuisha kabisa kama ilivyo dhamira ya serikali.

Daktari  ELIKANA amesema pamoja na kuwepo kwa baadhi ya wahudumu wa afya kuwauzia dawa za maralia wagonjwa na wengine kutumia  lugha mbaya pindi wanapowahudumia wagonjwa jambo jingine amesema ni ucheleweshaji wa usambazaji wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya Afya jambo ambalo linaashiria kupunguza kasi ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa maralia.

Hivi karibuni waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto  UMMY MWALIMU amewaagiza waganga wakuu wa mikoa kote nchini kuandika ubao wa matangazo katika hospitali utakaomjulisha mwananchi kuwa huduma ya malaria inatolewa bure na kuwa ni kipimo kipi kinatumika kupima malaria huku waganga wakuu wa wilaya na zahanati wakiagizwa kutoa namba zao za simu kwa ajili ya kupokea malalamiko ya wagonjwa iwapo watahudumiwa tofauti na maelekezo kutoka kwa wahudumu.


Na RWEIKIZA KATEBALIRWE                              Chanzo:DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...