Skip to main content

VIWANJA 10,864 MJINI DODOMA VINAUZWA ILI KUWAPA NAFASI WATU NDANI YA MAKAO MAKUU


                     
Image result for Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Godwin Kunambi


Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma imewatangazia wananchi wa Dodoma kwamba  imeanza zoezi la uuzaji wa viwanja 10,864 ili kuwapatia fursa na nafasi ya kununua viwanja ndani ya Makao Makuu ya Nchi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Dododoma GODWIN KUNAMBI amesema  mpango huo wa kutangaza ugawaji wa viwanja ni endelevu na lengo lake ni kumuwezesha kila mwananchi apate fursa ya kununua kiwanja.

Kunambi amesema mpango wa Upimaji wa viwanja ulianza mwezi January mwaka 2018 hivyo ni kazi ya miezi minne na wanatarajia kufikia mwishoni mwa mwezi huu jumla ya viwanja kumi na tisa elfu mia nne tisini na saba viwe vimeshapimwa.

Amesema maeneo yalinayopimwa viwanja hivyo ni IYUMBU ambapo vimepimwa viwanja 967, Mtumba viwanja 9897, Michese 1500 pamoja na Nara viwanja 7000 na tayari viwanja elfu 13 vimekamilika kwa upimaji.

Zoezi la uuzaji wa viwanja litafanyika katika Jengo la zamani la halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kuanzia  April 20 mwaka huu ili kuweka uwazi na uhuru na kila mwananchi anunue kwa haki bila kufanyiwa upendeleo.

Na Phina Nimrod                                              Chanzo:Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...