Skip to main content

VIONGOZI WATAKIWA KUENZI KWA VITENDO YALIYOFANYWA NA NA MWALIMU NYERERE

          Image result for KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE


Waziri wa nchi ofisi ya Makamu wa Rais muungano na mazingira Mh. January Makamba amewataka viongozi wa taifa wakiwemo vijana kutekeleza kwa vitendo mambo yaliyofanywa na waasisi wa Taifa kwa kuepuka vitendo vya rushwa pamoja na uchu wa madaraka.

Mh. Makamba ameyasema hayo leo katika kongamano la kumbukizi ya mwalimu Julius Kambarage Nyerere iliyofanyika katika Chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali.

Waziri makamba amesema Hayati Baba wa Taifa enzi za uhai wake alijitoa kwa dhati kulitumikia taifa bila kujali masilahi binafisi huku akipiga vita vitendo vya rushwa, uonevu, ubinafisi mambo ambayo viongozi wa sasa wanapaswa kutafakari iwapo wanayafanyia kazi na kuleta maendeleo kwa wananchi.

Kwa upande wake mzee Joseph Butiku aliewahi kufanya kazi na mwalimu Julius Kambarage Nyerere amesema taifa linahitaji kuboresha utoaji wa elimu iliyo bora kwa wananchi ili kurahisisha uendeshaji wa shughuli mbalimbali kwa wananchi pamoja na swala la taifa kujitegemea ili kukuza uchumi wake.

Nae mwenyekiti wa bodi ya chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere Prf. Mark Mwandosya amesema mwalimu Nyerere alijua kuwa nchi huendeshwa kwa mipango na kwamba mipango hiyo ni lazima itekelezwe ikiwa ni pamoja na kuepusha makundi mambo ambayo viongozi wa sasa wanapaswa kuyaishi.

Kongamano la kumbukizi ya mwalimu julius kambarage nyerere imeandaliwa na chuo cha kumbukizi ya Mwalimu Nyerere ikiwa ni kumbukizi ya kuzaliwa kwake mnamo tarehe 13.4.1922 katika wilaya ya Butiama Mkoani Mara.

Na Pius Jayunga                                                             DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...