Skip to main content

VIONGOZI WA MITAA NA KATA DODOMA WASISITIZWA KUSIMAMIA USAFI WA MAZINGIRA

Wito umetolewa kwa viongozi wa kata zote  na mitaa mbalimbali mkoani  Dodoma  kuhakikisha zoezi la usafi wa mazingira katika maeneo yao linafanyika kwa ufanisi.


Wito huo umetolewa na Afisa mazingira wa manispaa ya Dodoma Bw. Dicksoni Kimaro wakati akizungumza na Dodoma ambapo amewataka viongozi wa ngazi za mitaa na kata kutumia vyeo vyao ipasavyo kwa kusimamia wananchi ili kuhakikisha mji unakuwa katika hali ya usafi.

Ametoa wito huo mara baada ya baadhi ya maeneo mkoani hapa kuonekana kushindwa kuondoa taka zilizopo katika maeneo yao ambapo wananchi wake wameshindwa kulipia pesa kwa muda muafaka kwaajili ya kubebewa taka na kupelekwa sehemu husika.

Akizungumzia maeneo ambayo bado kuna changamoto kubwa katika ulipaji wa pesa kwaajili ya kubebewa taka miongonui mwao ni mtaa wa FM, SWAY,pamoja na KIKUYU ambapo amewataka viongozi wa mitaa hiyo kuzichukulia hatua za haraka  changamoto hizo ili waweze kukabiliana nazo.

Na kwa upande wake Afisa Afya Idara ya usafi na mazingira Bw.JOHN STEVEN LUGENDO ameitaka jamii kuachana na matumizi ya mashimo kwaajili ya kuhifadhia taka na badala yake watumie vifaa maalmu vilivyowekwa kwaajili ya kuhifadhia taka ili kuepusha taka kusambaa na kusababisha magonjwa ya mlipuko.

Sanjari na hayo wananchi wametakiwa kubadilika kuendana na wakati ikiwa ni pamoja na kushirikiana katika swala zima la usafi wa mazingira pamoja na  uhifadhi wa taka katika vyombo vya kuhifadhia taka na sio kuchimba mashimo kama ilivokuwa kipindi cha nyuma.

Na ANIPHA RAMADHAN                                          CHANZO:DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...